Wednesday, 3 September 2014

YAJUE MADHARA YA KULALA NA NGUO ZA NDANI

Madaktari na waalamu wa afya wanashauri kulala bila nguo za ndani wakati wa usiku ili kuwezesha viungo vya uzazi kupata hewa ya kutosha ili kuepuka maambukizi ya fangasi na kutoa harufu mbaya katika sehemu za siri. Kuvaa nguo za ndani wakati wa kulala usababisha kubana sehemu za siri na joto kupita kiasi ambayo usababisha joto kupita kiasi na unyevu na kuvutia ukuaji wa fangasi na bakteria kwa jinsia zote huku pia zikisababisha upungufu wa mbegu za kiume na harufu mbaya.

Tuesday, 2 September 2014

KAMA UNASUMBULIWA NA MAUMIVU YA MGONGO

Maumivu chini ya mgongo hutokea sana kwa kila mtu na mara nyingi huwa ni chini ya mbavu za nyuma na juu ya miguu na huweza kusambaa mpaka kwenye kiuno na hips. Maumivu haya usikika na kuumiza pale unapoinua kitu, kusimama, kukaa kwenye kiti au kutembea na usababishwa na matumizi kupita kiasi ya misuli, kano, mishipa na neva za mgongoni au kwenye pingili za uti wa mgongo kutokana na kugandamizwa sana. Pia huweza kusababishwa na kuvunjika au maambukizi katika pingili za uti wa mgongo,  umri mkubwa, saratani ya mifupa,uzito kupita kiasi mawe katika figo, uvimbe na saratani ya kizazi .

KAMA UNASUMBULIWA NA KIUNGULIA MARA KWA MARA


Kiungulia ni maumivu makali yanayochoma na kuuguza sehemu za koo au kifua. Maumivu haya huweza kusababishwa na matatizo kama vidonda vya tumbo, ujauzito, matatizo katika koromeo, aina fulani ya vyakula, sigara, pombe, uzito mkubwa na hernia ambayo husababisha tindikali inayosaidia mmeng'enyo wa chakula kutoka tumboni hadi kwenye koromeo na kusababisha maumivu haya.

UMUHIMU WA KUOTA JUA ASUBUHI



Watu wengi huwa na upungufu wa vitamini D kwasababu hawatoki nje kupata mwanga wa jua ambao huchochea seli katika ngozi ya mwili wako kuzalisha Vitami D inayoboresha afya ya mifupa na meno na kukukinga na hatari ya kushambuliwa na  magonjwa ya moyo, kisukari na saratani. 

MAMBO YANAYOSABABISHA UPUNGUFU AU UKOSEFU WA MBEGU ZA KIUME

Ni vigumu sana kugundua dalili na ishara za ukosefu au upungufu wa mbegu za kiume kwani tendo la ndoa uendelea kufanyika kawaida na kutoa shaawa zisizokuwa na mbegu za kiume au zenye upungufu ambazo usababisha utasa kwa wanaume. Yafuatayo ni mambo ambayo huweza kusababisha tatizo ili na kumfanya mweza akose ujauzito kwa muda mrefu.

JINSI YA KUTUNZA NGOZI ZENYE MAFUTA

Ngozi yenye mafuta kwa kawaida huwa inang'ara, nene na yenye rangi iliyotitia. Mara nyingi ngozi yenye mafuta mengi sana huwa na chunusi nyingi na vipelepele na mara nyingine huwa na chunusi zenye vichwa vyeusi. Katika aina hizi za ngozi mafuta hutokana na tezi za sebaceous na kuzalisha mafuta zaidi ya kiwango kinachotakiwa. Mafuta hayo husambaa katika ngozi na kuifanya iwe na mafuta mafuta.

Monday, 1 September 2014

TATIZO LA KUTOKWA NA DAMU KWENYE FIZI

Mara nyingi kuvimba au kutokwa na damu kwenye fizi huweza kusababishwa na magonjwa mbalimbali ya kinywa na meno ambayo husababishwa na kutofanya vizuri usafi wa meno kwa usahihi  au maambukizi ya bakteria ambao usababisha utando mgumu kwenye meno. Utando huu hauwezi kutolewa kwa kupiga mswaki bali kwa kutumia vifaa maalumu na wataalamu wa meno. Pamoja na maambukizi au kutofanya usafi pia kutokwa na damu kwenye fizi usababishwa na magonjwa ya damu, kupiga mswaki kwa nguvu, ukosefu wa vitamini C na K.

.