Friday 11 September 2015

KAMA UNASUMBULIWA NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA UKOSEFU WA HAMU YA TENDO LA NDOA.

Kabla hutujafika mbali kama wewe hauna ndoa basi ishia hapa hapa. Elimu iliyopo ni kwa ajili ya walio ndoani tu. Wewe kijana nenda kacheza kiduku kwanza.

Kuna mambo mawili: Kwanza – Upungufu wa nguvu za kiume na, Pili – Ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa.

Upungufu wa nguvu za kiume ni ile hali wakati kila kitu kiko sawa uume hausimami kabisa, au unasimama lakini unatoa maudenda kibao, upo legelege na ukiingia kwenye uhondo haumudu mchezo. Hapa ikumbukwe ya kwamba mwanaume unakuwa na hamu lakini mstahiki meya hataki kutimiza wajibu wake. Mara nyingi wanaume wenye matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume wanakuwa hivyo kwa muda mrefu. Na wana aibika sana.

Ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa unawahusu jinsia zote mbili wa kiume na wa kike. Hapa ni kwamba wastahiki memeya wote (ME & KE) wanakuwa safi kabisa isipokuwa hawapokei chaji (network down) inahitaji boosting, yaani mwanamke akiguswa tu anahisi kaguswa na gunia la misumari. Mwanaume ndio usiseme hata mwanamke ajilengeshe vipi anaona kama sinema hivi. Hali hii hutokea katika vipindi vifupivifupi kwa wanaume na muda mrefu kwa wanawake hasa wenye umri kuzidi miaka 40 , na vipindi vufupivifupi kwa baadhi ya wanawake wa umri chini ya miaka 40

Sasa wewe mwanaume ukiwa na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kabla hujanywa dawa za virutubisho hakikisha, umepima, umetibu na kupona magonjwa ya presha na sukari. Unaweza tumia dawa zenye kemikali au za virutubisho vyovyote itakavyo kuwa lakini laiti upone magonjwa hayo kwanza ndio uanze dozi ya kuongeza nguvu za kiume na hamu ya tendo la ndoa.

Ikiwa utatibu tu upungufu wa nguvu za kiume bila kutibu magonjwa hayo na kubadili tabia tambua ya kwamba matatizo yako ya nguvu za kiume yatarudia tena. DOKEZO muhimu hapa ni kwamba magonjwa ya presha na kisukari yanapunguza nguvu za kiume na pia madawa ya kemikali yanayotumika kutibu presha na kisukari yanaongeza uwezekano wa wewe kuwa na upungufu wa nguvu za kiume. Kwa hiyo ni bora kabisa ukatumia virutubisho muhimu kwa ajili ya kujitibu taratibu presha na kisukari na hatimaye utibu upungufu wa nguvu za kiume
Pia utalazimika kuangalia ini na figo kama zinafanya kazi vizuri, ikiwa hazifanyi kazi vizuri ni LAZIMA utibu pia ili mwili wako uanze upya – Engine Overhaul.

Ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa unasababishwa na vitu mbalimbali lakini pia inaweza kuwa ni dalili za upungufu wa nguvu za kiume. Ikiwa utakuwa na ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa kwa baadhi ya siku au vipindi vifupi basi usiwe na wasiwasi, pata kirutubisho kinachoweza kukusafisha mwili wako na kuondoa sumu mwilini, kukupa nguvu uchangamke, lala vizuri, kula vizuri, fanya mazoezi na ondoa msongo wa mawazo.
Kwa wanawake pia jipatie kirutubisho kizuri kitacho sawazisha homeni zako za mwili, kuondoa msongo wa mawazo, vipindi vizuri vya hedhi, kukoma kwa hedhi ambako sio rafiki na kuchangamsha mwili.
Hapo tatizo la ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa utakuwa umekwisha.

Ndugu zangu na rafiki zangu usijichanganye kukosa hamu ya tendo la ndoa na upungufu wa nguvu za kiume ni vitu viwili tofauti. Kwa hiyo namna y

a kurekebisha matatizo hayo ni tofauti. Mfano ukila machungwa 20 kwa siku unaweza rudisha hamu ya tendo la ndoa kirahisi sana.

Ukishapona unashauriwa ule vizuri chakula bora (ukizingatia sana vyakula vinavyo rekebisha tatizo lako moja kwa moja kama tikiti maji), kula dona na mbogamboga, acha mirungi, sigara na ulevi wa kupindukia, acha punyeto, fanya mazoezi, acha michepuko, pima maradhi ya ini, figo, presha na kisukari mara kwa mara. Usipate uvivu wa kula chakula bora, maji mengi pamoja na mazoezi, kama huna mwenzako na unahamu ya kupindukia tafuta mwenzio ili kuepusha madhara ya kupiga punyeto na kuharibu saikolojia yako ya mapenzi.

Kwa wale ambao wana matatizo sugu kiasi ya kwamba utumiaji wa chakula unaweza kuchelewesha kurekebisha matatizo hayo hapo juu na wanahitaji virutubisho kwa ajili ya kuongeza nguvu za kiume, kuongeza hamu ya tendo la ndoa (wanawake na wanaume), kuongeza ujazo wa mstahiki meya (ME) , kusafisha ini na figo. Ingia private massage tuongee kwa upana. Wale wengine tuendelee kuchangia mada kwa manufaa ya ndoa zetu

No comments:

Post a Comment

.