Sunday 25 May 2014

FAIDA NA AINA MBALIMBALI ZA MASAJI.




Masaji ni tiba mojawapo inayoweza kukusaidia kupunguza uchovu, maumivu, kupumzisha akili  na kurekebisha  mzunguko wa damu. Zifuatazo ni aina za masaji ambazo unaweza kufanya ili kuweka mwili wako katika hali nzuri


Masaji ya kutumia jiwe( Hot stone massage)
Hii ni aina ya masaji ambayo hufanywa kwa kutumia mawe laini na yenye joto kiasi kulainisha misuli na kupunguza maumivu kwa kuifanya misuli isinyae na kulegea
.
Masaji ya kutumia mafuta (Aromatherapy massage)
Masji hii ni maarufu na hutumika mara nyingi kwa kutumia mafuta maalumu(Aroma oil) na hupoza na kutuliza mwili uliochoka pia hupunguza mawazo na kutuliza akili, pia mafuta aina lavender na Rose au aina nyingine tofauti huweza kutumika kutokana na upatikanaji wake katika maeneo husika

Masaji katika tishu za ndani (Deep tissue Massage)
Hii hufanywa kwa nguvu ili kufikia tishu na misuli ya ndani kwa ajili ya kuondoa maumivu ya muda mrefu yanayosababishwa na magonjwa mbali mbali ya mifupa na misuli. Pia huweza kusaidia kuondoa makovu yatokanayo na kuumia kwa sehemu za ndani za mwili

Masaji ya miguu (Foot massage)
Hii hufanywa kwa kutumia ncha za vidole au kipande kidogo cha ubao kinachotumika kuweka pasha na kulainisha sehemu za miguu kuanzia unyayo mpaka kwenye magoti na kiunoni na mara nyingi huwa ni kwa ajili ya kupumzika na kujifurahisha ila huweza kuondoa maumivu kwa mama mjamzito anapokaria kujifungua na kupunguza mawazo.

Masaji ya mgongoni (Back massage)
Hii hufanywa kulainisha misuli na viungo katika sehemu ya mgongo ili kupumuzisha mwili na kusaidia mzunguko mzuri wa damu katika mabega na shingo. Hii pia ni rahisi kuliko zote kwani huweza kufanywa nyumbani bila maelekezo yoyote ya kitaalamu ukilinganisha na nyingine.

Masaji kwa wajawazito (Pregnancy massage)
Hii hufanywa na wataalamu wa afya kuondoa na kupunguza mawazo, maumivu na uvimbe huku akiwekwa katika mkao mzuri kuzuia madhara kwa motto.  Hata hivyo inashauriwa kutokufanya masaji hii kipindi cha miezi mitatu ya ujauzito na wale wenye matatizo ya kiafya.



KWA MSAADA ZAIDI BONYEZA HAPA AU ACHA COMMENT YAKO CHINI









No comments:

Post a Comment

.