Monday 14 April 2014

JINSI YA KUEPUKA VITAMBI VINAVYOSABABISHWA NA BIA



Mara nyingi tumezoea kuwaona watu wengi wanaotumia kinywaji cha bia wakiwa na vitambi. Hali hii husababishwa na upungufu wa proteini aina ya  Albumin ambayo hutoka nje ya mishipa ya damu na kuvuta maji maji  nje ya mishipa hiyo ambayo hujaa na kujikusanya sehemu za tumbo na miguu .

Hali hii huweza kuambatana na kukosa hamu ya kula, kiungulia cha mara kwa mara, kushiba mapema, kukoroma na kupumua kwa shida au maumivu ya tumbo na mgongo sambamba na mrundikano wa mafuta katika sehemu za tumbo.
Pia pombe huharibu na kuingilia kazi za ini ivyo kupunguza hutengenezwaji wa aina hii ya protein pamoja na kuongeza presha katika mishipa ya damu ya ini(portal vein) ambayo ulazimisha maji kurudi na kujaa tumboni.
Matatibabu yake ni pamoja na kuacha au kupunguza kiasi cha pombe kwa siku pamoja kutumia dawa za Diuretics kama Lasix na Aldactone ambazo utolewa hospitali kwa ajili ya kupunguza maji yaliojaa tumboni ambayo baadae huweza kupelekea kuvimba miguu na kusababisha madhara katika sehemu nyingine za mwili kama mapafu. Kibovu na moyo hivyo kupelekea magonjwa mbalimbali.
Pia sindano kubwa hutumika katiaka hospitali za kisasa kuondoa maji maji yaliojaa tumboni kwa njia ya Paracentesis.
 

No comments:

Post a Comment

.