Wednesday 7 January 2015

FANYA YAFUATAYO KILA SIKU KWA AFYA BORA YA MWILI WAKO.

1. Jiwekee utaratibu wa kufunga kwa siku mbili au tatu, wakati huo ukitumia maji ama juisi ya matunda au vyote kwa pamoja. Usile chakula kingine chochote. Faida ya kufunga ni kuondoa sumu mwilini, ambazo mara nyingi zimekuwa chanzo cha magonjwa.


2. Wakati matibabu yanaendelea usitumie vyakula vya kuhamasisha mwili kama chai, kahawa, pombe, sigara, vinywaji vyote vya ‘cola’, vyakula vilivyokaangiziwa viungo vingi, nyama, mafuta yanayopatikana kwa wanyama, vyakula vya unga uliolowekwa na sukari nyeupe.

3. Epuka vyakula vilivyosindikwa (tinned) kwa kuwa havina virutubisho vya kutosha. Pia madawa yanayotumika kuvifanya vikae muda mrefu bila kuharibika yanaathiri mwili.

4. Pata muda wa kutosha kwa ajili yamapumziko na mazoezi.

5. Usinywe maji wakati unaendelea kula. Kunywa maji saa moja kabla na baada ya mlo.

6. Kunywa maji mengi iwezekenavyo. Usinywe chini ya glasi 8 kwa siku.

7. Tumia zaidi chakula cha mboga za majani, matunda, nafaka zisizokobolewa, aina zote za kunde, maharage na karanga, asali na maziwa.

8. Wakati wa usiku usikae muda mrefu ukisoma ama kutazama runinga. Mwanga usio wa asili huleta athari. Lala mapema.

9. Nenda kulala angalau masaa mawili baada ya chakula cha jioni.

10. Wakati unapokuwa umekaa ama unatembea, uti wa mgongo ukae wima.

11. Lalia godoro gumu wala siyo godoro ama kitanda kinachonesanesa.

12. Sagisha mboga na matunda kwa ajili ya kachumbari kwa maji ya moto ama yanayotiririka. Katakata matunda na mboga katika vipande vikubwa ili kuepuka kupoteza vitamini muhimu na madini.

13. Usile wakati umekasirika, una wasiwasi, una woga ama una majonzi

No comments:

Post a Comment

.