Wednesday 12 March 2014

Kama unahisi Maumivu wakati wa tendo la ndoa dawa iko hapa

KUVIMBA kwa kuta za uke kutokana na kushambuliwa na fangasi (candida albicans ) au bakteria. Kuta hizi huanza kuwa na vijitundu vidogo vidogo na kadiri muda unavyokwenda bila kutibiwa vitundu hivi huongezeka ukubwa na kuwa kama vidonda na hatimaye kuta za uke kuanza kumomonyoka na hali hii huondoa kabisa hamu ya kushiriki tendo.
Matatizo ya shingo ya kizazi (cervical incompetence) kutokana na maambukizi ya fangasi maeneo hayo. Kutoka kwa mbegu za kiume muda mfupi au masaa kadhaa baada ya tendo ni dalili kuu ya tatizo hili. Pia mwanaume anapogonga shingo hii ya kizazi mwanamke huwa kama anatoneshwa kidonda. Hali hii ya mbegu kurudi nje husababisha mwanamke kutoshika ujauzito.

Kuwa na uvimbe kwenye mji wa mimba/mfuko wa uzazi( Uterus). Uvimbe huu kitaalam hujulikana kwa majina mengi lakini `fibroid` ni maarufu zaidi. Huanza kama mbegu ndogo ya mchicha na hukua kubwa kama boga kubwa. Mwanamke huongezeka ukubwa wa tumbo na baadae huonekana kama ana mimba kubwa na watu hushangaa kwa nini hajifungui kipindi chote.
Maumivu wakati wa tendo hasa chini ya kitovu huashiria tatizo kwenye mirija ya uzazi. Yawezekana ikawa ni tatizo la mirija ya uzazi kujaa maji machafu kutokana na kuzaliana sana eneo hilo, tatizo ambalo hujulikana kitaalamu kama Hyrosalpinx.
Kitu hiki husababisha mirija ya uzazi kuziba kwani maji haya huwa mazito, kitu ambacho hupelekea mayai ya uzazi na mbegu za kiume kushindwa kupenya. Kutoshika mimba kwa mwanamke aliye kwenye ndoa au mahusiano kwa zaidi ya mwaka mmoja na anasikia maumivu ya aina hii ni kiashiria kikubwa cha tatizo hili.Pia kuna tatizo la kuvimba kwa kuta za mirija ya uzazi yaani Salpingitis. Hili pia husababisha mirija kuziba kama lisipotibiwa mapema. Vyanzo vya tatizo hili tutajifunza siku zijazo.
Maumivu wakati wa tendo chini ya kitovu pia huashiria tatizo la mwanamke kuwa na mrundikano wa vijivimbe vingi kwenye vifuko vya mayai ya uzazi.Kitaalam linaitwa Polysystic Ovarian Syndrome (PCOS )au Stain Livingthal Syndrome.
Kama mwanamke anasikia maumivu haya na wakati huo huo anaona siku zake za hedhi zinapishanapishana sana, na pia kuona uchafu kama maziwa mtindi unatoka ni dalili kubwa ya tatizo hili na hasa kama anaviashiria vya kuwa na homoni nyingi za kiume mfano kuwa na ndevu au vinyweleo vingi mikononi na miguuni.

No comments:

Post a Comment

.