Thursday 13 March 2014

Tiba asili ya Maumivu ya tumbo:

Watu wengi wamekuwa wakisumbuliwa na tumbo lisilo la vidonda wala ugonjwa wowote ila utasikia anakwambia tumbo linanikata, huenda akawa anavurugikwa na tumbo au imetokea linasumbua tu.


SOMA NA HII: Tiba ya maumivu wakati wa tendo la ndoa
Tiba hii hapa
Kwanza kabisa kama wewe unapenda kutumia vinywaji vikali ‘Alcohol’,  kahawa na vinywaji vyote vyenye ‘Caffeine’ jitahidi kuacha kwani inaweza kuwa sababu ya wewe kusumbuliwa na tumbo.
Lakini kama tumbo ni ugonjwa unaokusumbua mara kwa mara, kwanza chunguza katika hospitali kuhakikisha huna tatizo kubwa la kutibiwa kabla ya kujipa huduma za kinyumbani ‘Natural Remedies’.
Lakini ukishagundua huna tatizo kubwa huduma ya kwanza unayoweza kufanyiwa nyumbani ni hii hapa.
Kunywa chai yenye  mchanganyiko wa Tangawizi, ‘chamomile’ na majani ya nanaa.
Limao nayo inasaidia, unaweza kukatakata vipande na kunyonya maji yake kama unavyokula chungwa, au unaweza kuweka kwenye glasi ya maji ya vuguvugu  na kunywa.
Kula Yogurt
Kula maziwa aina ya yogurt, haya yanasaidia kuliweka sawa tumbo lako hasa pale linapokuwa kwenye hali ya kuvurugika. Kwa kufanya hivyo unaweza kusafisha kwa kutoa uchafu tumboni au kukata kwa maumivu tu.
Hapa kwenye yogurt epuka yenye sukari nyingi jaribu kula yenye ladha ya vanilla ni nzuri zaidi, kumbuka kinywaji hiki kina tibu mambo mengi kwani mbali na tumbo pia husaidia kutibu msongo wa mawazo na kuweka sawa akili
Tangawizi pekee
Chukua tangawizi isage kamua maji yake kisha weka kwenye kinywaji chochote chaweza kuwa cha baridi au cha moto ni dawa pia.
Epuka kula vyakula vizito usiku mwingi
Vyakula hivyo husababisha tindikali kwenye tumbo na hufanyika pale usiku unapokula haraka na kupanda kitandani bila kukipa nafasi chakula kuyeyuka tumboni.
Kumbuka wakati mzuri wa kula chakula ni kati ya saa mbili usiku mpaka saa nne na baada ya hapo usipande kitanda wakati huohuo jaribu kujipa nafasi kwa ajili ya kuruhusu chakula kifike eneo husika na kianze kusagwa ndiyo ulale.
Wengine hufanya zoezi la kutembea baada ya chakula ili kukipa nafasi nzuri ya kufanya kazi.
Utakuta mtu anakula viazi au wali maharagwe na jamii ya vyakula vingine vizito kisha hajipi muda wala hanywi maji anadandia kitanda kisa amechelewa kulala, hii ni sumu ndani ya tumbo lako kwani nafasi ya kufanya kazi inakuwa ndogo sana.
IMETOKAhttp://www.dullonet.com/afya/tiba-asili-ya-ugonjwa-wa-tumbo/

No comments:

Post a Comment

.