Tuesday 4 March 2014

TUNDA LA STAFELI LINA UWEZO WA KUTIBU MAGONJWA HATARI:

Tunda la stafeli kuwa na uwezo mkubwa wa kutibu magonjwa hatari, ukiwemo ugonjwa wa saratani. Hata hivyo, utafiti wa kwanza kuonesha uwezo wa stafeli kutibu saratani, uligundulika tangu miaka ya sabini, lakini ulifanywa siri hadi hivi karibuni ulipowekwa bayana tena.

Hivi sasa wakereketwa wa tiba mbadala na dunia kwa ujumla, wanafahamu kuwa stafeli lina virutubisho vyenye uwezo mkubwa wa kutibu magonjwa ya saratani kushinda hata dawa za kisasa. Tunda hili linapatikana nchini kwa wingi, mjini na vijijini. Kwa lugha za kigeni linajulikana pia kama Soursop au Graviola.
VIRUTUBISHO VILIVYOMO
Kwa mujibu wa tafiti za kisayansi, stafeli limesheheni idadi kubwa ya virutubisho ambavyo ni: Amino Acid, Acetogenins, Vitamin C, Iron, Riboflavin, Phosphorus, Thiamine, Calcium, Carbohydrates, Niacin na Fibers na vingine vingi.
SARATANI NA STAFELI
Ingawa suala la stafeli peke yake kutibu saratani lina mjadala, lakini hakuna shaka kabisa kuwa lina virutubisho vyenye uwezo wa kupambana au kupunguza makali ya saratani. Ukweli uliogundulika hivi karibuni, umewapa wagonjwa wa saratani njia nyingine mbadala ambayo haikuwepo hapo awali. Kwani hivi sasa wanaweza kulitumia stafeli kama dawa ya kupunguza makali au kuwapa kinga dhidi ya saratani na wanaweza pia kuitumia pamoja na matibabu wanayopewa ya mionzi na kupata ahueni kubwa.
USHAHIDI WA KIMAABARA
Zaidi ya majaribio 20 ya kimaabara yaliyofanywa kuhusu uwezo wa stafeli, yamebaini haya yafuatayo:
Stafeli huua chembechembe za saratani (cancerous cells) aina 12, ikiwemo saratani ya matiti, mapafu, kongosho, kibofu na tumbo.
Stafeli lina mchanganyiko wenye uwezo mkubwa wa kudhibiti ukuaji wa seli za saratani mara 10,000 zaidi ya dawa ya ‘Adriamycin’ ambayo ndiyo hutumika kutibu aina mbalimbali ya saratani.
Mchanganyiko wa virutubisho vya ‘Annonaceous’ ‘Acetogenins’ vilivyomo kwenye stafeli huua seli (cells) zilizoathirika tu na saratani, tofauti na dawa za kisasa ambazo zenyewe huua seli zilizoathirika na hata zisizoathirika.
Stafeli hudhibiti ukuaji wa seli za saratani bila kusababisha madhara mengine kama ilivyo kwa dawa za kisasa, ambazo wakati mgonjwa anapozitumia, iwe zile za njia ya mionzi, sindano au vidonge, huwa zina athari mbaya kwa mtumiaji na wakati mwingine huweza kumsababishia matatizo mengine ya kiafya.
UMUHIMU WA STAFELI KWA WANAOTUMIA TIBA YA KISASA
Mgonjwa wa saratani anayetumia tiba ya hospitali anashauriwa pia kula sana stafeli kwani lenyewe husaidia kupunguza makali ya dawa anazotumia.
Imetoka: http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/stafeli-lina-uwezo-wa-ajabu-wa-kutibu-magonjwa-hatari

No comments:

Post a Comment

.