Monday 15 December 2014

ATHARI YA MAGONJWA YA NGONO KWA MAMA NA MTOTO.

Athari za magonjwa ya ngono ni pamoja na kuharibika mimba mara kwa mara, mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi, ugumba, kuziba kwa mirija ya uzazi, madadiliko ya hedhi, kujifungua kabla ya mimba kutimiza muda wake, kansa ya uume,
kupungua nguvu za kiume, utasa, kuziba njia ya mkojo, magonjwa ya akili na maambukizi katika kokwa za mbegu za uzazi. Kwa upande wa watoto magonjwa haya husababisha mtoto adumae, uambukizo wa macho, upofu, kuzaliwa na uzito pungufu pamoja na vichomi.
Ili kujiepusha na magonjwa ya ngono, ni vyema mtu ukachukua tahadhari hizi, kuepuka ngono katika umri mdogo, kutumia kondomu wakati wa kujamiiana, kujiepusha na vitendo vya ubakaji. Pia ni vizuri kama unatibiwa magonjwa haya, basi na mwenzi wako pia umpeleke akapatiwe matibabu.

No comments:

Post a Comment

.