Monday 29 December 2014

MAZINGIRA TUNAYOISHI YANAVYOWEZA KUATHIRI AFYA ZETU

Mazingira ni jambo lingine linaloathiri afya. Iwapo maji tunayokunjwa na kutumia ni safi na salama, iwapo hewa tunayovuta si chafu, maeneo tunayofanyia kazi ni salama na pia nyumba tunazoishi, basi afya zetu huwa salama zaidi ikilinganishwa na watu wanaoishi kwenye maeneo yasiyo na maji safi na salama au kuvuta hewa chafu na kufanya kazi kwenye mazingira ya hatari. 

Uchunguzi uliofanywa na chuo kikuu cha Zuyd nchini Uholanzi umeonesha kwamba, kuvuta hewa iliyochafuliwa kwa gesi za magari kwa lisaa limoja kunatosha kumpatia mtu mfadhaiko wa kifikra au stress katika ubongo wake. Utafiti mwingine uliofanywa na chuo kikuu cha India cha Purdue umebainisha kuwa, sumu kali inayotokana na sumu ya risasi, inayoweza kuiingia mwilini mwa binadamu kutokana na kula vitu vilivyoingiwa na sumu hiyo, nchini Marekani huathiri maelfu ya watoto kuliko kiwango dhaifu cha sumu hiyo kinachoweza kuwepo katika vifaa vya kuchezea na mapambo yanavyosafirishwa.
Afya ya binadamu pia huweza kuathiriwa na watu wanaomzunguka. Iwapo una familia unayoiangalia au marafiki katika jamii yako, basi una nafasi kubwa ya kuimarisha afya yako kuliko mtu ambaye anaishi pekee au hana familia na marafiki. Uchunguzi uliofanywa na chuo kikuu cha Washington nchini Marekani umegundua kuwa, ushirikiano wa kifamilia ni jambo zuri kwa mtu na hupunguza kesi za atu kujiua, hasa wale wanaopatwa na matatizo ya mfadhaiko wa kifikra au wanapokuwa na fikra ya kutaka kujiua.  Vilevile tamaduni, mila na desturi za jamii na jinsi watu wanavyozithamini itikadi hizo, zina mafasi kubwa katika afya zao ingawa matokeo yake huweza kuwa mazuri au mabaya. Kwa mfano mazoea na mila ya kuwakeketa au kuwatahiri watoto wa kike na wanawake ina madhara makubwa kama vile kuongeza kiwango cha maambukizo ya magonjwa na hata matatizo ya kiakili miongoni mwa wasichama na wanawake wanaofanyiwa jambo hilo. Utafiti uliochapishwa katika Jarida la Afya ya Jamii na  Elimu ya Magonjwa ya Mlipuko umebainisha kuwa, wakati vijana wanapovaa mavazi kwa mujibu wa mila na tamaduni za makundi au makabila yao, suala hilo huweza kuwapunguzia uwezekano wa kupatwa na matatizo ya kiakili baadaye maishani.

No comments:

Post a Comment

.