Thursday 18 June 2015

Soma Madhara ya Sigara na Uyaepuke

Kuvuta sigara ni tabia ambayo imezoeleka na watu wengi ingawa ina madhara mengi Uvutaji sigara huathiri mwili kwa njia tofauti na madhara yake ni makubwa kiafya. Inakadiriwa kuwa, hadi sasa kumegunduliwa kemikali zipatazo 7,000 katika moshi wa sigara ambapo 250 kati ya hizo ni sumu na 70 zinasababisha kansa. 


Mvutaji mdogo hutumia nusu ya pakiti ya sigara kwa siku na kujikuta akiathiri mwili wake kwa kemikali hizi mara 3500 kwa mwaka. Mada na kemikali zilizo kwenye sigara huathiri karibu kila kiungo mwilini kuanzia seli hadi mfumo wa kulinda mwili.
 Kemikali zilizoko kwenye moshi wa sigara huingia katika mapafu na kuenea katika mwili mzima na kusababisha madhara makubwa kwa njia mbalimbali. Ingawa mada hizo haribifu zilizoko kwenye moshi wa sigara ni nyingi, lakini tatu ni hatari zaidi zikilinganishwa na nyingine. Mada hizo ni nikotini, carbon monoxide na tar.

BOFYA HAPA KUJUA MARADHI MENGINE YANAYOSABABISHWA NA SIGARA 

No comments:

Post a Comment

.