Wednesday 15 October 2014

JINSI YA KUCHAGUA VIPODOZI SAHIHI KWA AFYA YA NGOZI YAKO.

Katika chapisho HILI tuliongelea kuhusu madhara ya vipodozi endapo havitatumika kwa usahihi.
Kabla hujaanza kutumia vipodozi ni vyema ukajua aina ya ngozi yako kwa usahihi kabisa na uwezo wa kumudu ghalama za vipodozi kwa muda wote. Hapa lazima ujue kama ngozi yako ni kavu, yenye mafuta,mchanganyiko ,au una ngozi ambayo ni rahisi kupata chunusi.
Baaada ya kujua aina yako ya ngozi ni vyema ukaingia katika hatua nyingine ya kuchagua vipodozi vyenye ingredients sahihi kwa ajili ya ngozi yako. Lakini kwa aina zote za ngozi, vipodozi vyote vyenye sunscreen na antioxydants ni muhimu sana kwa ajili ya ustawi wa ngozi yako.
Epuka kutumia vipodozi vyenye ingredients ambazo ni hatari kiafya na zimepigwa marufuku na serikali, mfano saizi epuka kutumia vipodozi ambavyo vina kemikali za ‘hydroquinone’ na corticosteroids
Kwa mtu mwenye ngozi yenye mafuta anatakiwa kutumia vipodozi ambavyo vipo katika’ base’ ya liquid au gel,ambavyo vinaweza kuwa na ingredients kama vile Benzoyl peroxide,maji mengi,salicyclic acid na kadhalika, kwa kitaalamu anatakiwa atumie water based cometics, wakati mtu mwenye ngozi kavu anatakiwa atumie vipozi ambavyo vina unyevu na mafuta mengi ambavyo vipo katika ‘base’ ya lotion,cream na kadhalika.
Kwa hiyo uchaguzi mzuri wa vipodozi ni jambo ambalo kila mtu anapaswa kulijua ili kupelekea muonekano mzuri, ambao utakuwa mchango mkubwa katika afya ya mtu kwa namna moja au nyingine.

BOFYA HAPA KULIKE PAGE NA UNGANA NASI FACEBOOK KWA MSAADA ZAIDI

No comments:

Post a Comment

.