Sunday 12 October 2014

SOMA KUHUSU MUHUDUMU WA AFYA ALIYEFARIKI KWA EBOLA NA UCHUKUE HATUA.

Mfanyakazi aliyemtibu mgonjwa wa Ebola Thomas Eric Duncan  nchini Marekani kabla hajafariki asemekana kukutwa na virusi vya Ebola kutokana na utafiti wa afya aliofanyiwa. Mfanyakazi huyo ambaye jina lake limehifadhiwa amewekwa kwenye kitengo maalum inasemekana kwamba alivaa mavazi maalum ya kumkinga na ugonjwa huo wa Ebola.
Untitled
Duncan ambaye alipata virusi hivyo vya Ebola alipokuwa mjini Liberia alifariki Jumatano. Mlipuko huo vya virusi vya Ebola kutoka miji ya Liberia,Guinea na Sierra Leone imethibitishwa kuwa na waathirika 8300 na vifo vya kukaribia 4033.

Hospitali imethibitisha kuwa njia za kujikinga na maambukizi hayo ya Ebola zinafatwa kwa auangalizi mkubwa na wafanyakazi wote ambao wanafanya kwenye kituo hicho cha afya cha Texan Health Presbyterian. Mkuu wa kituo hicho cha afya Dr. Tom Frieden (CDC) alisema kuna uwezekano mfanyakazi huyo hakufata njia zote husika za kujikinga na ugonjwa huo.
1
Mkuu wa kituo hicho cha afya alikiambia chombo cha habari cha Marekani CBS kwamba watafanya uchunguzi ili kujua ni jinsi gani muhudumu huyo wa afya alipata virusi hivyo vya Ebola. Alisema wafanyakazi wote ambao walimuhudumia Duncan watafanyiwa uchunguzi ili kujua kama na wao wamepata virusi hivyo vya Ebola.
CHANZO: http://millardayo.com/

No comments:

Post a Comment

.