Saturday 11 October 2014

VYAKULA VINAVYOFAA KWA MAMA MJAMZITO.

Madaktari wengi wanashauri kunywa madawa ya vitamin sababu wajawazito wengi hawali vizuri. Madini ya muhimu kwa mtoto ni kama yafuatayo; Calcium, Iron, Folate (B vitamin). Haya madini yote yanaweza kupatikana kwenye vyakula vifuatazo;



Calcium:
Mtoto anahitaji Calcium kwa ajili ya kukuza viungo vya mwili na mifupa kukomaa vizuri. Mwili wako unanyonya Calcium inayohitajika na mtoto hivyo basi unahitaji kula vyakula vitakavyoongeza kiasi hichi mwilini. Lakini pia ili Calcium inyonywe na mwili unahitaji kukaa juani kwa kipindi kama cha dakika kumi kila siku. Calcium hupatikana kwenye, maziwa, mboga za majani kwa wingi, Mayai (Hakikisha yameiva vizuri )Samaki (esp mifupa lakini sio samaki wote wanashauliwa kula wakati wa mimba), maharage ya soya, na mchele.

Madini ya Chuma (Iron)
Chuma ni muhimu kwa utengenezaji wa damu, kwani kipindi hichi damu nyingi inahitajika kwa ajili ya kumpelekea mtoto chakula. Wajawazito wengi huwa vichanga vyao vinakufa sababu ya ukosefu wa damu toka kwa mama. Iron hupatikana toka kwa vyakula kama; Mboga za majani kwa wingi zaidi (Matembele yana Iron zaidi, mchicha, brocolli, sukuma wiki n.k). Chai na Kahawa huwa inasaidia kuzuia kunyonywa ka iron mwilini hivyo epuka kunya chai nyingi na ikiwezekana uache kunywa kahawa kwa kipindi hiki.

CHANZO MTOTO NA AFYA

No comments:

Post a Comment

.