Tuesday 28 October 2014

MUUGUZI KUISHITAKI SERIKALI BAADA YA KUWEKWA KARANTINI YA EBOLA

Siku chache baada ya New York na New Jersey kutangaza utaratibu mpya wa kuwaweka karantini wauguzi na madaktari waliotoka kuhudumia wagonjwa katika nchi zilizoathiriwa na Ebola, muuguzi wa kwanza kuathiriwa na utaratibu huo Kaci Hickox ametishia kufungua mashtaka kutokana na kufanyiwa kitendo hicho.

Muuguzi huyo ameruhusiwa kurejea nyumbani kwao Maine, ambapo ameilalamikia karantini aliyowekwa mbali na kutoonekana kuwa na dalili za maambukizi ya Ebola baada ya kuwasili New Jersey na kutishia kufungua mashtaka kwa kudai kuwa kitendo alichofanyiwa cha kuwekwa karantini hakikuwa cha kibinadamu na ni kinyume na haki zake kikatiba.
Marekani inaendelea kuangalia namna ambavyo itaweza kuweka utaratibu mzuri wa kuwafuatilia kwa ukaribu watu waliotoka nchi za Afrika Magharibi, Guinea, Liberia na Sierra Leone.
Kituo cha udhibiti wa Magonjwa cha Marekani (CDC) kimetaka kuwepo utaratibu maalum wa kuwaweka wahudumu wa afya wanaorudi kutoka Afrika Magharibi katika karantini za nyumbani.

No comments:

Post a Comment

.