Wednesday 6 August 2014

TATIZO LA KIKOHOZI CHA MUDA MREFU.

Kukoa ni kitendo cha kuondoa uchafu au kamasi ili kusafisha njia ya juu ya hewa. Kikohozi cha muda mrefu ni kikohozi kisichopona kwa zaidi ya wiki 3 2 na kuendelea na huwa sio ugonjwa bali ni ishara ya ugonjwa au tatizo lililopo mwilini kama ifuatavyo:
PIA MADHARA YA KUKOSA USINGIZI
  • Uvutaji wa Sigara, kwa kawaida wagonjwa wengi wa kikohozi cha muda mrefu huwa ni wavutaji wa sigara na baadhi hupona pale wanapoacha na wengine huchelewa baada ya kuwa wamepata matatizo mengine makubwa katika njia ya hewa.
  • Ugonjwa wa pumu, ambapo njia ya hewa uvimba, kujaa maji na kuzuia mfumo wa upumuaji kufanya vizuri.
  • Ugonjwa wa kucheua na kiungulia(Gastro esophageal reflux disease) hii usababishwa na chakula ambacho kishaingia tumboni na kuchanganywa na tindikali kurudi kaika koo na hutokea mara nyingi usiku ambapo mtu hushindwa kupumua vizuri na kukooa sana.
  • Kuvimba mianzi ya pua, ambapo mtu uhisi kitu, kutekenywa au kuwashwa kooni na kukooa kwa muda mrefu.
  • Maambukizi, ambayo husababishwa na bakteria na virusi katika njia ya hewa kama pnemonia, kifaduro, na magonjwa mengine ya moyo na mapafu.
  • Matatizo mengine ambayo husababisha mara chache ni pamoja na Allergy, dawa za muda mrefu, saratani, TB, emphysema, mapafu kuanguka.
 Kumbuka kikohozi cha muda mrefu sio cha kupuuzia kwani huweza kusababisha maumivu makali ya kichwa, uchovu, jasho kupita kiasi, kushindwa kuzuia haja ndogo na kuvunjika mbavu.
WASILIANA NASI KWA MSAADA ZAIDI





No comments:

Post a Comment

.