Monday 8 September 2014

VYAKULA VITAKAVYOKUFANYA KUISI NJAA MUDA WOTE

Kuna baadhi ya watu wamehathirika na ulaji wa vyakula mbalimbali ambavyo hawawezi kuacha hata kama vinawaletea madhara. Kuna vyakula vingi ambavyo ukila utajisikia kushiba lakini utaISI njaa baada ya muda mfupi. Hivi ni baadhi ya vyakula hivyo

1. Kutafuna bigiji, Pipi au bablishi, hii huzalisha mate kinywani na juisi ambayo husaidia kusaga chakula kinywani na tumboni na kufanya tumbo lijae kwa muda mfupi na kukufanya huisi njaa baada ya muda mfupi.
2.  Kunywa Soda, kwa kawaida sukari ya asili hukufanya kusikia hamu ya kula wakati sukari iliyotengenezwa viwandani na inayopatikana kwenye soda huzuia seli katika mfumo wa fahamu wa tumbo(Enteric nervous system)  kukufanya uisi baada ya muda mfupi.
3. Kulamba Koni, koni ina kiwango kikubwa cha sukari aina ya fructose ambayo huingilia mfumo wa utendaji kazi wa mwili (Body metabolism) na kuzuia utoaji wa kemikali ya leptin ambayo hukujulisha kuwa umeshiba na acha kula hivyo kuendelea kula.
4. Vyakula vyenye ubaridi, kama matunda mboga za majani hukosa nyuzinyuzi na kutanua tumbo na kukufanya ushibe kwa muda mfupi.
5. Keki na mikate ya kuoka hii huwa na sukari nyingi na hukosa virutubisho na nyuzinyuzi hivyo kukufanya uisi kushiba na njaa baada ya muda mfupi. Unashauriwa kutumia keki zenye virutubisho na kiwango kidogo cha sukari
UNAWEZA KUTUSHIRIKISHA CHAKULA CHOCHOTE UNACHOHISI KIMESAHAURIKA KWA KUBOFYA HAPA 


No comments:

Post a Comment

.