Sunday 7 September 2014

VYAKULA MUHIMU SANA AMBAVYO UKIZIDISHA HUWA SUMU MWILINI.

Vifuatavyo ni vyakula muhimu sana kwa afya ya mwili wako ambavyo ukizidisha vinaweza kuwa hatari sana na kukusababishia maradhi mbali mbali.

1. Nyama ukila nyama kupita kiasi husababisha kiasi kikubwa cha protein na vichochezi vya ukuaji mwilini ambavyo huongeza kasi ya kuzeeka na hatari ya kupata saratani, kisukari na shinikizo la damu.
2. Samaki wa kwenye makopo, samaki hawa ambao wameshatengenezwa na upatikana kwenye maduka ya vyakula huwa na kiasi kikubwa cha mekuri ambayo ukizidisha inaweza kusababisha matatizo ya macho na upofu.
4. Machungwa na nyanya, kuzidisha kiwango cha nyanya na machumgwa mwili husababisha tumbo kujaa gesi na kusababisha uzalishwaji wa tindikali tumboni ambayo hurudi na kuharibu koromeo.
5. Maziwa, pamoja na kuwa na virutubisho vingi unywaji wa maziwa kupita kiasi husababisha kiasi kikubwa cha mafuta mwilini ambayo huziba mishipa ya damu na kusababisha matatizo ya moyo.
 UNGANA NASI FACEBOOK KUJUA MENGI ZAIDI

No comments:

Post a Comment

.