Thursday 11 September 2014

UNAWEZA KUMUHUDUMIA MGONJWA WA KIFAFA.

Utendaji mzuri wa ubongo unategemea uwiano katika kutuma ujumbe. Utumaji usio na udhibiti hupelekea mlipuko wa umeme katika seli za ubongo ambapo huweza kupelekea mtu kupata kifafa (seizure) hali ambayo huambatana na kupoteza fahamu,kuzubaa,kukakamaamisuli, kuchanganyikiwa, kutokwa na haja ndogo au kuchezesha viungo haswa mikono na miguu.

Sote tuko katika hatari ya kupata kifafa.Kifafa chaweza tokea bila sababu dhahiri lakini watu waliowahi kudhurika katika ubongo wako katika nafasi kubwa ya kupata kifafa. Kifafa hurithiwi mara chache haswa kwa ndugu ambao wana muathirika wa kifafa.

 Nini cha kufanya iwapo mgonjwa wa kifafa amepatwa na kifafa
1. Ondosha vitu vyovyote vinavyoweza kumdhuru kama moto, mawe, visu n.k
2. Usimuhamishe kumpeleka mahala pengine
3. Mgeuze upande (kiubavu) ili kama kuna kimiminika chochote mdomoni kiweze kutoka ili kuepuka kuziba kwa njia ya hewa.
4. Toa nguo yoyote inayombana shingoni ili aweze kupumua vizuri
5. Kaa naye mpaka apate fahamu (yaweza kuchukua mpaka dakika kumi na tano)
6. Wasiliana na wataalamu wa afya au mpeleke hosipitali iwapo hajapata fahamu baada ya dakika 5 mpaka 10
7. Usimwekee kitu chochote mdomoni wa usijaribu kumzuia mgonjwa asirushe mikono au miguu

BOFYA HAPA KUUNGANA NASI FACEBOOK 

No comments:

Post a Comment

.