Friday 5 September 2014

VYAKULA 10 VINAVYOFAA KWA WANAUME.



1. Chokolate, hurekebisha mzunguko wa damu na kuondoa mafuta ambayo hayafai kwenye mishipa ya damu hivyo kukuepusha na shinikizo la damu. Ila kula mara kwa mara itasababisha kuongezeka uzito.
2. Samaki kutoa baharini, asa wenye magamba ambao huwa na virutubisho vya zinc vinavyosaidia kuimarisha misuli, moyo na utoaji wa mbegu za kiume. Pia vyakula kama karanga, nyama ya ng’ombe na kukuk huwa na kiasi kikubwa cha madini haya.

3. Parachichi, tunda ili huwa na mafuta mazuri ambayo husaidia kuondoa mafuta yenye athari katika mishipa ya damu na hivyo kuzuia magonjwa ya moyo.
4. Tangawizi, kutafuna tangawizi mara kwa mara hupunguza maumivu ya misuli yanayotokana na kufanya kazi nzito au kuumia.
5. Maziwa, huwa na kiasi kikubwa cha protein na potassium ambayo husaidia kujenga  misuli imara. Pia ina bacteria rafiki wanaosaidia kulinda mfumo wa chakula na kuzuia vidonda vya tumbo.
6. Ndizi mbivu, Ina virutubisho vya potassium ambavyo uimarisha misuli, mifupa na kupunguza shinikizo la damu.
7. Nafaka, vyakula hivi huongeza nguvu na huwa na nyuzinyuzi kusaidia kupata choo vizuri na kuimarisha mwili wako.
8. Tomato Souce ina virutubisho vya leukopene ambavyo ukulinda dhidi ya saratani ya tezi ya kiume.
9. Mboga za majani na matunda, kama pilipili, machungwa,  karoti, spinachi na maboga zina kemikali na virutubisho vinavyosaidia kuongeza kinga ya mwili, kuzuia kuzeeka mapema na kukukinga na saratani.
10. Mayai, yana virutubisho vya lutein, protini namadini ya chuma yanyosaidia ukuaji wa chembe nyekundu za damu.




No comments:

Post a Comment

.