Thursday 4 September 2014

MATUMIZI YA SIGARA ZA UMEME NA MADHARA YAKE

Watafiti wa afya kutoka Marekani wameonya matumizi ya sigara za kielektroniki zilizoandaliwa kuwasaidia wavutaji sigara kuacha uvutaji kwamba zinaweza kuwatumbukiza katika matumizi ya dawa za kulevya.

Wanasema kuwa sigara hizo aina e-cigarettes ni kweli zinaweza kupunguza madhara ya uunguaji wa tumbaku lakini zinaweza kuleta madhara makubwa kama yale ya nicotine inayopatikana katika tumbaku.
Watalaam hawa wanasema mabadiliko ya mchangaiko huo unaweza kuleta madhara katika ubongo na pia unaweza kuwa chanzo cha hamasa kwa mtu kuvutiwa matumizi dawa za kulevya kama vile coccaine.
Ripoti ya utafiti iliyochapishwa katika jarida la the Journal of Medicine inasema madhara yanaweza kuwa makubwa zaidi kwa makundi ya vijana.
CHANZO BBC

No comments:

Post a Comment

.