Wednesday 17 September 2014

UNAWEZA KUEPUKA MADHARA YANAYOSABABISHWA NA UNENE KUPITA KIAS (Obesity)



Unene kupita kiasi husababishwa kuwa na  mafuta mengi  mwilini kutokana na  kukosa mazoezi ya kutosha au kula chakula kupita kiasi ambacho ukosa matumizi na kuifadhiwa kwenye tumbo, makalio, maziwa au kiungo chochote laini. Hii pia inaweza kuchangiwa na mabadiliko ya hormone asa kipindi cha ujana, uzeeni au ujauzito na kurithi katika familia.

Tatizo ili hukuweka katika hatari ya kupata magonjwa ya moyo na ini, kiharusi, shinikizo la damu,  kisukari, kukoroma usiku, maumivu katika joint za mifupa,  kushindwa kupumua vizuri na saratani.
MATIBABU YAKE
1. Kupanga lishe na mazoezi ni tiba tosha ya tatizo ili. Epuka vyakula vyenye mafuta na sukari nyingi na kula vyenye nyuzinyuzi , matunda na nafaka.
2. Juice ya limao glasi moja kila asubuhi ni njia raisi ya kupambana na unene huu kwani hurekebisha mfumo wa chakula, damu na kuondoa sumu mwilini.
3. Juisi ya mshubiri ikichanganywa na machungwa kila asubuhi kwa muda wa mwezi mmoja husaidi kuondoa mafuta ya ziada mwilini.
4. Kijiko kimoja cha asali katika kikombe cha chai kila siku husaidia kupunguza mafuta mwilini.
5. Unaweza pia kupunguza kulala mchana, kukaa kwenye sofa au kukalia viti laini kwa muda mrefu
Kunywa maji ya moto badala ya baridi husaidia kuondoa mafua ya ziada kwenye mishipa ya damu.
LIKE PAGE YETU FACEBOOK USIPITWE NA MENGI ZAIDI KUHUSU AFYA YAKO.



No comments:

Post a Comment

.