Sunday 9 November 2014

UMUHIMU WA KIFUNGUA KINYWA KWA AFYA YAKO



Utafiti uliofanywa na wanasayansi wa masuala ya afya na lishe nchini Marekani umebaini kuwa “kifungua kinywa huupa moyo afya na kuuepusha na magonjwa ya mshtuko wa moyo.” 

Utafiti wao uliowahusisha wanaume 27,000 wenye umri kati ya miaka 45-82 ulionyesha kuwa wale wasiokula kiamsha kinywa wako katika hatari ya matatizo ya moyo. Wakati wa utafiti huo, zaidi ya watu 1,500 waliathirika kutokana na mshtuko wa moyo.
Utafiti huo ulithibitisha kuwa watu waliokosa kifungua kinywa wako katika hatari kubwa ya kupata matatizo ya moyo kwa asilimia 27 kuliko wale wanaokula asubuhi.
Ukizingatia utafiti uliofanywa na Chuo kikuu cha Harvad kitivo cha afya ya jamii kilisema kuwa: “kukosa kiamsha kinywa kunasababisha mwili kutumia nguvu nyingi zaidi kuliko kawaida.” Sambamba na utafiti huo, taasisi ya matibabu ya moyo nchini Uingereza imebaini kuwa “kiamsha kinywa huwazuia watu kula vitu vyenye sukari kabla ya chakula cha mchana.”(http://www.bbc.co.uk/swahili/kwa_kina/2013/07/130723_kiamsha_kinywa.shtml).
Kupata kifungua kinywa kwa mtu wa kipato cha chini inawezekana...si lazima iwe kama picha inavyoonyesha, ni muhimu kuzingatia makundi ya vyakula unayotakiwa kula kulingana na kipato chako.Yote tisa, kifungua kinywa ni muhimu sana kwa afya yako.

No comments:

Post a Comment

.