Sunday 2 November 2014

UNAWEZA KULINDA MENO YAKO YASIOZE KWA KUFANYA YAFUATAYO.

1: KUPIGA MSWAKI:
  • ·      Piga mswaki kwa daikika 2 angalau mara mbili kwa siku.
  • ·      Ni nyema kupiga mswaki kabla ya kulala kwani ulinzi wa meno kwa mate yako ni mdogo ukilinganisha na uwapo macho.
  • ·      Kupiga mswaki baada ya kula ni mazoea mazuri, hukinga uchafu utoknao na chembe za chakula kujijenga kati kati ya meno yako.
  •  

2: KUTUMIA ‘MOUTH WASH’:
  • ·      Tafuta na tumia ‘Mouth Wash’ uipendayo kuyapa nguvu meno yako.
  • ·      Soma maelekezo kan-bla ya matumizi.
  • ·      Wafundishe watoto kati ya miaka 6 -12 jinsi inavyotumiwa  ili wasiimeze.
  • ·      Kumbuka ‘Mouth wash ’ haimezwi.



3: UCHAGUZI WA VYAKULA SAHIHI:
  • ·      Chagua vyakula vyako kwa makini.
  • ·      Epuka kula kula ovyo, jambo linaloongeza uchafu utokanao na vyakula kwenye meno.
  • ·      Epuka vyakula vyenye sukari na vinavyonata, vyakula vya aina hii utengeneza mazingira ya bakteria kuzaliana kwa winigi mdomoni.
  • ·      Pata mlo sahihi (Balance diet ) kwa ulinzi wa meno yako. Mfano ni maji mengi, mboga mboga, matunda, maziwa nk.
  •  

4: KUONANA NA DAKTARI WA MENO:
Jenga tabia ya kuonana na tabibu wa meno angalau mara moja kwa miezi sita na kila uhisapo maumivu ya meno kwa ajili ya utafiti na usafi wa meno yako

No comments:

Post a Comment

.