Friday 14 November 2014

USICHOFAHAMU KUHUSU KUTOA USHUZI.

Kutoa ushuzi au Kujamba kunasababishwa na kubanwa kwa hewa,ambayo inaweza kutoka mwilini  kwa njia nyingi.Baadhi ni hewa tuliyoimeza wakati wa kula au  kunywa.Hewa ingine husababishwa na gesi kuingia kwenye utumbo wetu  kutoka kwenye damu,na baadhi ya gesi huzalishwa na kemikali katika  utumbo au bakteria.Kwa kawaida "ushuzi" unakua na asilimia 59 ya gesi ya  nitrogen,
asilimia 21 ni hydrogen,asilimia 9 ni carbon dioxide,asilimia 7  methane na asilimia 4 ni oygen. Asilimia moja tu ya "ushuzi" inaweza kuwa  hydrogen sulfide na mercaptans,ambayo ndio ina sulfur ndani yake,sulfur  ndo hufanya "ushuzi" utoe harufu mbaya  Kujamba huambatana na sauti,hii ni kutokana na "vibration" katika njia  ya haja kubwa.Ukubwa wa mlio wa kujamba hutegemea "presha" inayosukuma  gesi itoke nje na pia ugumu wa misuli ya njia ya haja kubwa.
Harufu mbaya ya ushuzi hutegemea na ulaji wa mtu,vyakula vyenye sulfur  kwa wingi ndio husababisha hili.Vyakula vyenye sulfur kwa wingi ni kama maharage,kabichi,soda na mayai.

Kwa Baadhi ya Tamaduni,Kujamba Sio Ishu
Wakati tamaduni nyingi zikichukulia tendo la kujamba lifanywe  kistaarabu,kuna baadhi ya tamaduni hawaoni haya kujamba hadharani,na pia  hufurahia tendo hilo.Mfano kabila la Yanomami huko America ya  Kusini,kwao husalimiana kwa kujamba,na China unaweza kupata kazi ya  kunusa ushuzi! Katika Roma ya zamani,Mfalme Claudius akihofia kwamba  kujizuia kujamba inaweza kuwa hatari kiafya,alipitisha sheria kwamba ni ruhusa kujamba kwenye "banquets". 

Mtu wa kawaida hutoa hata nusu lita ya ushuzi kwa siku.Inasemekana mtu  akijamba mfululizo kwa kipindi cha miaka 6,anaweza kuzalisha nishati ya  kutosha kutengeneza bomu la atomiki.

No comments:

Post a Comment

.