Saturday 1 November 2014

JITIBU CHUNUSI KWA KUTUMIA TUNDA LA PARACHICHI.

Vinavyohitajika:
1.Avocado moja lililoiva vyema.
2.Mtindi kijiko kimoja cha chakula.
3.Asali asilia (natural honey).
4.Maji ya ndimu/limao.


Namna ya kutayarisha:
Kata Avocado katika vipande viwili, ondoa kokwa na menya.
Changanya avocado ulomenya na mtindi, asali na maji ya ndimu au limao. Koroga mapaka upate mchanganyiko wa hali moja halafu weka pembeni.
Chukua maganda ya avocado na kwa upande wa ndani ya maganda hayo sugulia uso na shingo. Kufanya hivyo husaidia kuondoa seli zilizokufa na ngozi zilizoharibika. Pia huutayarisha uso kwa ajili ya mask.
Kisha paka mchanganyiko uliotayarisha usoni na shingoni (sio machoni).
Subiri kwa dakika 15 na kisha osha kwa maji vuguvugu.
 Usitumie mask ya Avocardo kama ngozi yako ni yenye mafuta na kutoka chunusi. Kwani Avocado kwa kuwa na mafuta mafuta, maska ya tunda hilo hufaa zaidi kwa wenye ngozi kavu na za kawaida. Kwa ajili ya ngozi zenye mafuta unaweza kutumia mask zinazotengenezwa kwa udongo, ndizi,tango, chai na kadhalika.
BOFYA HAPA KULIKE PAGE NA WAELIMISHE MARAFIKI 

No comments:

Post a Comment

.